TANZANIA LOCAL GOVERNMENT WORKERS UNION

Talgwu Chama Imara, Huduma bora kwa Wanachama.

Kuhusu sisi

Dhima yetu

Kuunganisha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa kwa ajili ya kupigania uwepo wa huduma bora, uboreshwaji wa huduma za kiuchumi na kijamii, uwepo wa maendeleo endelevu ya kitaaluma na kitaalam, na kuimarisha nguvu ya pamoja ya majadiliano, ili kufikia kuwa jamii yenye usawa kupitia Uongozi bora

Dira yetu

Kuwa Chama cha Wafanyakazi chenye ufanisi mkubwa  na kinachojitegemea nchini Tanzania.

Je madhumuni ya kuanzishwa TALGWU ni yapi?​

  • Kupigania na kuwahimiza waajiri kuboresha hali nzuri ya wanachama katika maisha yao wakiwa kazini na wakati wa kustaafu.
  • Kujadiliana na kuondoa tofauti kati ya waajiri na wanachama kwa njia ya majadiliano ya amani.
  • Kusimamia na kushauri katika uundaji wa mikataba ya hali bora mahali pa kazi.
  • Kuwasiliana na serikali kuhusu utungaji wa sheria sahihi za kazi na kuandaa sera nzuri za kuendeleza uchumi na maisha.
  • Kulinda maslahi ya wanachama kwa kuwasiliana na serikali ili kuepukana na uandaaji wa sera ambazo ni hatari kwa wanachama.

Kwanini ujiunge na TALGWU?​

  • Ili kuwa na umoja katika kupigania haki na maslahi yao.
  • Kupata uwakilishi katika vyombo vya maamuzi.
  • Kupata msaada wa kisheria pale wanapokumbwa na migogoro kazini.
  • Kuelimishwa kuhusu masuala mbalimbali ya kiutumishi.