Tanzania Local Government Workers Union
Viongozi Wakuu wa Chama
Mwenyekiti Taifa
Katibu Mkuu
Makamu Mwenyekiti
Kaimu Katibu Mkuu
Mweka Hazina
Kuhusu Chama
TALGWU ni Chama cha wafanyakazi wa serikali za Mitaa Tanzania ambacho kimesajiliwa chini ya sheria ya vyama vya wafanyakazi no 10 ya mwaka 1998,na kilipewa nambari ya usajili 010 tarehe 15/09/2000. TALGWU inaunganisha wafanyakazi wote waliopo chini ya Mamlaka za serikali za mitaa na Taasisi nyingine nchini ambapo hadi kufikia June 2024, Chama kilikuwa na wanachama 89,100.TALGWU inajishirikisha na shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) shirikisho la vyama vya wafanyakazi vinavyotoa huduma kwa umma duniani (PSI) na Mtandao wa Vyama vya Wafanyakazi vya Serikali za Mitaa Africa (AMALGUN). Hivyo basi chama cha wafanyakazi ni ummoja, muungano, na mshikamano wa wafanyakazi ambao nia, malengo, matakwa na matarajio yao yanafanana.Umoja huo ndio nguzo pekee ya kupatia ufumbuzi wa matatizo yao. TALGWU inaelimisha, inatetea, na kulinda ajira na ujira wa wanachama wake kwa kuzingatia sheria, taratibu, kanuni, miongozo na nyaraka mbalimbali za kazi
Tangazo
Tangazo la Tenda kwa mwaka 2027
Mitandao
Sheria
Kuwatetea wafanyakazi katika migogoro, mashauri na kesi pindi wanapokuwa kazini
Uwakilishi
Kuwawakilisha Wafanyakazi katika majadiliano ya pamoja na Serikali /Waajiri.
Elimu
Kuwaelimisha Wanachama kuhusu wajibu wao mahala pa kazi ili kuleta tija na kuongeza uzajishaji.
Usimamizi
Kusimamia maslahi ya Wanachama katika njia ambayo itawahakikishia ustawi wao wa kitaaluma na kiuchumi
Kuanzisha na kudumisha uhusiano na ushirikiano na wadau wengine
Kuendelea Kushirikiana na kubadilishana ujuzi na vyama vingine vya wafanyakazi nchini pamoja na vile vya kimataifa kwa lengo la kuboresha maslahi ya wanachama wake.
Kutoa elimu kwa wanachama kuhusu wajibu wao mahala pa kazi
Kuhimiza wafanyakazi kufanya kazi kwa bidii na uadilifu wanapotekeleza majukumu yao ya kila siku. Pia kuwaelimisha kuhusu Sheria, Kanuni na Taratibu zinazotumika nchini.
Kuwatetea wafanyakazi katika mashauri na kesi kazini
Kutoa huduma za kiutumishi na kisheria kwa wanachama wake pale wanapokuwa na changamoto za kesi, migogoro ama mashauri pindi wanapokuwa kazini.
Kuwatetea wafanyakazi katika mashauri na kesi kazini
Kutoa huduma za kiutumishi na kisheria kwa wanachama wake pale wanapokuwa na changamoto za kesi, migogoro ama mashauri pindi wanapokuwa kazini.




