Huduma zetu
Ni muda sasa wa kujiunga na TALGWU
Katika kufikia malengo ya Chama tuliyojiwekea ya kutoa huduma bora kwa Wanachama wetu (quality public services), mnamo mwezi januari 2018, Baraza Kuu Taifa lilipitisha mpango mkakati wa Chama wa miaka minne. Utakaojikita katika kuboresha huduma zetu.

Kulinda na kuoanisha mazingira na hali bora ya kazi kwa Wafanyakazi wote wa Mamlaka za Serikali za Mitaa
TALGWU itajikita katika tafiti zenye lengo la kubaini uwiano wa mishahara kati ya Watumishi wa Serikali za Mitaa na sekta nyingine ili kupata msingi wa majadiliano na Mwajiri. Chama kitajenga misingi ya majadiliano ya pamoja na Serikali juu ya mishahara bora kwa Wafanyakazi, pamoja na kumshawishi Mwajiri kuboresha Ofisi wanazotumia Wanachama wetu na kutoa vitendea kazi.

Kukifanya Chama kuwa msemaji mkuu kwa niaba ya Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa kutoka ngazi ya Taifa hadi chini
ambapo Chama kitaongeza idadi ya Wanachama kutoka 67% ya wafanyakazi wote wa Serikali za Mitaa kwa sasa hadi 95% ya wafanyakazi wote wa Serikali za Mitaa ifikapo mwaka 2022 pamoja na kufikia kuwa na mbinu ya pamoja katika kushughulikia masuala yote yanayoathiri utoaji wa huduma bora kwa Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa .

Kuendeleza ustawi wa kusimamia maslahi ya Wanachama katika njia ambayo itawahakikishia ustawi wao wa kitaaluma na kiuchumi
Chama kitalinda na kutetea maslahi ya Wanachama wetu katika kipindi chote cha utekelezaji wa mpango mkakati huu. Aidha Chama kitandelea kuifadhili TALGWU MICROFINANCE PLC ili iweze kukopesha Wanachama wengi zaidi pamoja na kudumisha hadhi ya ustawi wa kiuchumi na kijamii ya Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa

Kuanzisha na kudumisha uhusiano na ushirikiano na wadau wengine
ambapo Chama kitaendelea kuimarisha uhusiano uliopo kati yake na Vyama vingine vya Wafanyakazi na wadau mbalimbali ndani ya nchi, Kikanda na Kimataifa pamoja na kuendeleza na kudumisha mahusiano na mashirikiano mengine kwa maslahi ya Wanachama wetu ..
Kwanini TALGWU ?
- Kupigania na kuwahimiza waajiri kuboresha na kuendeleza hali nzuri ya wanachama katika maisha yao wakiwa kazini na wakati wa kustaafu.
- Kuwasiliana na serikali kuhusu haja ya kutunga sheria sahihi za kazi na kuandaa sera nzuri za kuendeleza uchumi na maisha ya jamii.
- Kuishauri Serikali kupunguza kodi ya mishahara ya mfanyakazi.
- Kusimamia na kushauri katika uundaji wa mikataba ya hari bora mahali pa kazi.
Kwanini wafanyakazi wa Serikali za Mitaa wajiunge na TALGWU ?
- Ili kuwa na umoja katika kupigania haki na maslahi yao.
- Kupata uwakilishi katika vyombo vya maamuzi.
- Kupata msaada wa kisheria pale wanapokumbwa na migogoro kazini.
- Kuelimishwa kuhusu masuala mbalimbali ya kiutumishi.